Uhali gani mpenzi msomaji wa mtandao huu unaokujuza mengi yaendeleayo madhabahuni mwa Bwana GRC Ubungo Kibangu.
Kama kawaida katika kila siku ya Alhamisi kama ya leo, huwa kuna ibada ya maombezi ambayo hungozwa na mtumishi wa Mungu, Mchungaji Antony Lusekelo, ambapo katika siku ya leo, somo kuu lilikuwa ni juu ya kibali.
Hizi ndo sifa za kibali, kibali utengenezwa na nini, na baadhi ya watu waliyokuwa na kibali katika Biblia
Sifa za kibali;
Humpa mtu kusikilizwa, kuaminika, kupendwa, kuthaminika n.k
Kibali hutengenezwa na nini?
Kibali hutengenezwa na tabia ya mtu binafsi, mfano kwa kuwa na roho nzuri, tabia nzuri, kujituma, kujali, msafi, n.k.
Baadhi ya watu waliyokuwa na kibali katika Biblia.
Daniel - Na ndiyo maana kibali hicho kilisababisha Nebukardeza mfalme wa nchi, kumsujudia.
(Soma Daniel 3)
Yusufu- Ndiyo maana alipelekwa kwa Potifa kama mtumwa ili ajifunze uongozi.
Musa- Ndiyo maana akapata nafasi ya kuingia katika ikulu ya Farao na akapata elimu ya kutosha uongozi.
Baada ya somo hilo zuri maombezi ya nguvu yaliendelea na tulimsifu sana Mungu kwa pamoja na Mzee wa Upako.










