Mwanzo 1:20

Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.

Mwanzo 1:12

Nchi ikaota majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake,na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Zaburi 24:1-2

Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake. Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari, Na juu ya mti ya maji aliithibitisha.

Yoeli 2:1

Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Pigeni na kelele katika mlima wangu mtakatifu; Wenyeji wote wa nchi na watetemeke; Kwa maana siku ya Bwana inakuja. Kwa sababu inakaribia.

Yeremia 1:18-19

Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo za chuma, na kuta za shaba; juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii. Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema BWANA, ili nikuokoe.

Thursday, February 13, 2014

KIBALI

Watashindana! Lakini hawatashinda.

Uhali gani mpenzi msomaji wa mtandao huu unaokujuza mengi yaendeleayo madhabahuni mwa Bwana GRC Ubungo Kibangu.

Kama kawaida katika kila siku ya Alhamisi kama ya leo, huwa kuna ibada ya maombezi ambayo hungozwa na mtumishi wa Mungu, Mchungaji Antony Lusekelo, ambapo katika siku ya leo, somo kuu lilikuwa ni juu ya kibali.

Hizi ndo sifa za kibali, kibali utengenezwa na nini, na baadhi ya watu waliyokuwa na kibali katika Biblia

Sifa za kibali;

Humpa mtu kusikilizwa, kuaminika, kupendwa, kuthaminika n.k

Kibali hutengenezwa na nini?

Kibali hutengenezwa na tabia ya mtu binafsi, mfano kwa kuwa na roho nzuri, tabia nzuri, kujituma, kujali, msafi, n.k.

Baadhi ya watu waliyokuwa na kibali katika Biblia.

Daniel - Na ndiyo maana kibali hicho kilisababisha Nebukardeza mfalme wa nchi, kumsujudia.
(Soma Daniel 3)

Yusufu-  Ndiyo maana alipelekwa kwa Potifa kama mtumwa ili ajifunze uongozi.

Musa- Ndiyo maana akapata nafasi ya kuingia katika ikulu ya Farao na akapata elimu ya kutosha uongozi.

Baada ya somo hilo zuri maombezi ya nguvu yaliendelea na tulimsifu sana Mungu kwa pamoja na Mzee wa Upako.