Thursday, August 1, 2013

Mjue vyema Nguli huyu wa Injili hapa nchini.

Mzee wa upako

Anajulikana kwa jina la Mzee wa Upako, Katapila, Transformer, pamoja na majina mengi ambayo amekuwa akipatiwa na waumini wake kutokana tu na nguvu alizonazo za maombi (upako), zinazowafungua watu wengi katika matatizo mbalimbali. Yeye ni baba wa watoto wanne ambao ni Modekai, Salome, Mishaeli, pamoja na Elishadai.  Mkewe ni Bi.Happiness Ngasala, moja kati wa wafanyakazi wa TBC Taifa, huku wote wakiwa ni Wanyakyusa.
Katapila yeye ni mcheshi, mkali kiasi, mkweli, si mnafiki, jasiri katika yale anayoyaamini, pamoja na muwazi huku akiwa na mapenzi ya kweli kwa kila ampendaye na mwenye kuiamini Injili yake.
Katika mahubiri yake, mara zote huyachambua katika hali ya uhalisia huku akionyesha wazi kukerwa na umasikini tuliyonao Watanzania pamoja na Waafrika kwa ujumla.
"Watashindana lakini hawatashinda, tutapanga mipango, itapangika, wakituloga imekula kwao na kwetu hakuna kudumaa", ni baadhi tu ya misemo ya Biblia, inayomtambulisha vyema Mchungaji huyu.

0 comments:

Post a Comment