Marehemu Askofu Kulola akihubiri.
Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu imezipata kutoka kwa watu wa ndani wa familia hiyo, zinaeleza kuwa Askofu Kulola amefariki katika hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam.
Askofu Kulola, ambaye amezaliwa mwaka 1928, amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu na hata kufikia hatua ya kupelekwa nchini India kwa matibabu.
Katika uhai wake, amepata watoto wengi wa kiroho ikiwemo Dr Daniel Kulola, Mchungaji Florian Katunzi, Zakaria Kakobe, Maboya, Mwasota na wengineo wengi.
Blogi hii itaendelea kukufahamisha kwa kadri ambavyo taarifa zitakuwa zikitufikia.Kufahamu historia ya maisha ya Hayati Askofu Dr. Moses Kulola
BWANA ametoa na BWANA ametwaa, jina la BWANA lihimidiwe.







0 comments:
Post a Comment